Shirika lisilo la faida lililoko - Tanzania

Kuwawezesha wanafunzi, walimu na watu wote ambao wanahitaji ujuzi wa TEHAMA kufanya kazi KIDIGITALI.

TEHAMA KWA WOTE

Ilianzaje?

Wakati Powercomputers ikikamilisha miaka 20 kwa upande mmoja na kwa kuzingatia wazo la kusaidia jamii na serikali kwa upande mwingine, tuliamua kuanzisha mradi wa ICT FOR ALL - TEHAMA KWA WOTE kwenye hafla ndogo na wafanyakazi wangu.

Tumesajiliwa chini ya sheria ya NGO Tanzania kwa usajili wa namba 00NGO/R/2884

Tunatarajia kubadilisha maisha ya watanzania kupitia NGO hii..

Tunachodhamiria kufanya

Kukuza matumizi ya TEHAMA

Kukuza matumizi ya TEHAMA katika sekta mbalimbali zikiwemo elimu na utoaji wa elimu.

Kutoa elimu juu ya matumizi ya teknolojia

Kutoa elimu juu ya matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano katika shughuli za kila siku za mtu.

Rasilimali muhimu kwa elimu ya TEHAMA

Kukuza utoaji wa rasilimali muhimu kwa elimu ya TEHAMA kwa watu.Hii inajumuisha utoaji wa vifaa mbali mbali kama computers, mashine za kutoa kopi. N.K

Kujenga ufahamu

Kujenga ufahamu kwa watu juu ya umuhimu wa TEHAMA na kwenda sambamba na teknolojia inayobadilika kwa kasi.

Kutoa msaada katika tasnia ya TEHAMA

Kutoa msaada katika tasnia ya TEHAMA katika masuala ya vifaa na programu..

Rasilimali muhimu kwa elimu ya TEHAMA

Mafunzo kwa waalimu ya TEHAMA

Kutoa mafunzo kwa waalimu ya TEHAMA katika elimu na kuibua uwezo wa TEHAMA katika utoaji wa elimu.

200

Walimu waliofundishwa

6

Maabara za TEHAMA

600

Wanafunzi wa Kidato cha IV waliofunzwa

50

Mikutano na mikusayiko

100

Shule zilizotembelewa

Tehama Kwa Wote in Tanzania

Lengo letu ni kuongeza uwezo na kukuza uelewa wa teknolojia ya habari na mawasiliano kwa jamii ya Kitanzania.

Kwa hakika, tunaishi katika ulimwengu wa kidijitali unaoendelea kubadilika. TEHAMA inagusa kwa karibu kila nyanja ya maisha yetu - kutoka kazini hadi kijamii, kujifunza na kucheza.

 

Enzi ya kidijitali imebadilisha jinsi vijana wanavyowasiliana, kujuana, kutafuta msaada, kupata taarifa na kujifunza. Ni lazima tutambue kwamba vijana sasa ni watu wa mtandaoni, wanaopatikana kupitia njia mbalimbali kama vile kompyuta, televisheni na simu za mkononi.

swSW